YANGA SC wamebainisha kuwa msimamo wao kuhusu mchezo wa Kariakoo Dabi dhidi ya Simba SC uliotarajiwa kuchezwa Machi 8 2025 upo palepale.
Yanga imebainisha kuwa msimamo wao upo palepale kuhusu mchezo huo licha ya CAS kutoa majibu ya kesi yao kuhusu kesi ya mchezo huo.
Taarifa iliyotolewa na Yanga SC Mei 5 2025 imeeleza namna hii: “Uongozi wa Yanga unapenda kuutarifu umma kuwa umepokea majibu kutoka Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhishi wa Michezo, (CAS) kuhusu kesi namba CAS 2025/A/11298.
“CAS imeilekeza Yanga SC kurudi kwanza kwenye Kamati za ndani za soka ili kushughulikia kesi hiyo kabla ya kurudi kwao kwa ajili yah atua za rufaa.
“Lakini kutokana na uonevu, uvunjwajwi mkubwa wa kanuni na upendeleo wa dhahiri kwa baadhi ya timu unaoendelea kufanywa na mamlaka za soka Tanzania, uongozi wa Yanga hauna imani na hauko tayari kupeleka shauri hilo kwenye mamlaka ambazo zinatenda dhuluma.
“Aidha uongozi wa Yanga unapenda kuujulisha Umma kuwa msimamo wa klabu ya Yanga upo palepale kuwa hautashiriki mchezo namba 184 wa ligi msimu wa 2024/25 uko palepale kuwa hawatashiriki kwenye mchezo huo kwa namna yoyote ile.
“Wanayanga wote watakuwa tayari kuipambania haki yao kivyovyote vile ili kukomesha dhuluma na uvunjwaji mkubwa mkubwa unaoendelea kufanywa na mamlaka za soka kwa maslahi mapana ya maendeleo la soka.”