KIMATAIFATETESI ZA USAJILI

MBWANA SAMATTA KUUNGANA NA MSUVA, SAUDI ARABIA

Nyota wa kimataifa wa Tanzania ๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ฟ anayecheza soka la kulipwa katika timu ya PAOK ya Ugiriki, Mbwana Samatta โ€˜Popatโ€™ inaelezwa anajiandaa kumfuata Simon Msuva anayecheza soka nchini Saudi Arabia ๐Ÿ‡ธ๐Ÿ‡ฆ baada ya klabu ya Al Kholood iliyopanda Ligi Daraja la Pili nchini humo kutuma maombi ya kumtaka nahodha huyo wa Taifa Stars kwa mkopo.

Kama dili hilo litakamilika huenda Samatta akakutana na pacha anayecheza naye Taifa Stars, Msuva anayeichezea Al Najma katika ligi hiyo. Samatta amekuwa na wakati mgumu wa kupata nafasi ndani ya kikosi cha PAOK na mkataba alionao na Wagiriki hao unatarajiwa kutamatika Juni, mwakani.

Related Articles

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button