mamelodi

Siku tatu kabla ya kurudiana na Yanga SC katika Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika (CAFCL), Mamelodi Sundowns leo majira ya saa 02:30 usiku, watakuwa wenyeji wa Richards Bay katika michezo ya Ligi Kuu ya Afrika Kusini (PSL), Uwanja wa Loftus Versfeld, jijini Pretoria.

Katika msimamo wa PSL, Mamelodi ni kinara wa msimamo akikusanya alama 46 katika michezo 18 huku wapinzani wao Richards Bay wakiwa nafasi ya 15, nafasi moja kutoka chini ya msimamo. Wamevuna jumla ya alama 14 katika michezo 21.

Wawakilishi wa Tanzania, Yanga SC wapo angani muda huu kuelekea Afrika Kusini kukabiliana na Mamelodi Aprili 05 Ijumaa hii katika Uwanja wa Loftus Versfeld baada ya suluhu tasa 0-0 katika mchezo wa awali Machi 30, 2024, Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam.

HABARI HIZI ZINAPATIKANA KATIKA APP YA SOKALEO, BONYEZA HAPA KUIDOWNLOAD

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here