KITAIFA
BAADA YA KUWA NJE MECHI MBILI, YAO BEKI KITASA AREJEA

Beki Yao Kouassi amerejea mazoezini baada ya kupona goti lililokuwa likimsumbua ambalo lilimfanya kukosekana katika mechi mbili za mwisho dhidi ya Vital’O na Kagera Sugar ambazo zote Yanga ilishinda.
Wakati Yao alipokosekana, Gamondi alibadili mfumo kwa kuwatumia mabeki watatu nyuma, lakini kupona kwake na akiwa fiti kucheza, basi atarejea katika mfumo wake wa kuwatumia mabeki wanne.