Feisal Salum

KIUNGO mshambuliaji wa Azam FC, Feisal Salum ameweka wazi kuwa bora ndani ya uwanja ni kufuata maelekezo ya mwalimu.

Fei amekuwa bora msimu wa 2023/24 akiwa na uzi wa Azam FC ni mabao 14 katupia ndani ya ligi akiwa namba moja kwa wazawa wenye mabao mengi.

Nyota huyo bao la 14 alipachika kwenye mchezo dhidi ya Ihefu ilikuwa dakika ya 13 na mwisho ubao wa Uwanja wa Azam Complex, Aprili 21 ulisoma Azam FC 1-0 Ihefu.

Nyota huyo amesema:”Kikubwa ni kufuata maelekezo ya mwalimu pamoja na ushirikiano uliopo kati ya wachezaji,”.

HABARI HIZI ZINAPATIKANA KATIKA APP YA SOKALEO, BONYEZA HAPA KUIDOWNLOAD

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here